https://www.ajol.info/index.php/kcl/issue/feed Kioo cha Lugha 2025-03-11T13:05:21+00:00 Dkt. Rhoda Peterson Kidami kidamis@yahoo.com Open Journal Systems <p><em>Kioo cha Lugha</em> is an international journal published by the Institute of Kiswahili Studies (IKS). The journal is devoted to the publication of papers on Kiswahili language, linguistics and literature and other African languages. It promotes critical discussions and reviews, especially on contemporary issues regarding language and literature. The journal also publishes short pieces of fiction and poems. It is published annually but from 2021 it will be published bi-annually.</p> <p>Journal website: <a href="https://journals.udsm.ac.tz/index.php/kcl" target="_blank" rel="noopener">https://journals.udsm.ac.tz/index.php/kcl</a></p> <p><br /><br /></p> https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/290874 Umbuji wa Watani katika Maombolezo ya Wangoni: Uchunguzi wa Vipengele Teule vya Fasihi 2025-03-11T10:57:21+00:00 Martina Duwe magriccola@gmail.com <p>Kiasili, Wangoni hutumia utani kama nguzo muhimu ya kufikisha maudhui lengwa kwa hadhira, hususani katika shughuli mbalimbali za kitanzia na kiramsa. Katika shughuli za kitanzia, mathalani, maombolezo; watani hutumia umbuji unaozingatia kaida zao ili kufikisha&nbsp; ujumbe fulani kwa hadhira husika. Umbuji huo huweza kubainika kupitia sanaa za maonesho, kama vile uchezaji wa ngoma na matumizi&nbsp; ya lugha ya kibunifu inayoambatana na vitendo mbalimbali kama uigizaji na uimbaji. Hata hivyo, haijawa bayana ni kwa namna gani&nbsp; uwasilishaji wa maudhui hayo kupitia vipera vya fasihi simulizi unabainisha umbuji unaosawiri maisha yao halisi. Kwa hiyo, makala hii&nbsp; inafafanua jambo hilo kwa kurejelea maombolezo ya jamii ya Wangoni. Haya ni matokeo ya utafiti uliofanyika katika mazingira halisi ya&nbsp; Wangoni. Data za utafiti huu zilipatikana kwa mbinu za ushuhudiaji katika matukio yanayoambatana na suala la mazishi pamoja na usaili.&nbsp; Vilevile, misingi ya Nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi imetumika kama mwegamo mkuu katika kuchunguza, kuchambua data na&nbsp; kuwasilisha matokeo ya utafiti. Matokeo yanaonesha kuwa watani katika maombolezo ya Wangoni wana dhima kubwa ya kufikisha&nbsp; maudhui kwa jamii kupitia umbuji unaosawiri utamaduni wao. Hivyo, makala hii inajadili umbuji huo kwa kujiegemeza katika vipengele&nbsp; teule vya fasihi simulizi ambavyo ni: maigizo, nyimbo na semi.&nbsp;</p> 2025-03-11T00:00:00+00:00 Copyright (c) 2025 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/290876 Miangwi ya Kimtindo, Kidhamira na Uhusika: Uchunguzi wa Kazi Teule 2025-03-11T11:03:56+00:00 Kyallo W. Wamitila wamitila@gmail.com <p>Makala hii inachunguza namna ambavyo kazi za kifasihi zinaakisi uhusiano na ufanano wa kimatini hasa katika kiwango cha mtindo, dhamira na usawiri na uendelezaji wa wahusika. Msingi wake mkuu ni imani kuwa fasihi inahusiana na fasihi na matini na kazi&nbsp; mbalimbali huingiliana, kuathiriana, kutagusana na kujalizana katika mwanda wa kimwingilianomatini. Matini za kimsingi ambazo&nbsp; zimechunguzwa ni tamthiliya mbili (Mashetani ya E. Hussein na Mashetani Wamerudi ya S.A. Mohamed), hadithi fupi ya “Mke Wangu” ya&nbsp; M.S. Abdulla na riwaya ya Wenye Meno ya S.A. Mohamed, zilizoteuliwa kimakusudi. Uchunguzi huo umefanywa kwa kuzingatia mawazo&nbsp; ya Nadharia ya Mwingilianomatini inayohusishwa na Julia Kristeva aliyebuni dhana hii mwaka 1966. Kristeva aliyakuza mawazo yake&nbsp; kwenye msingi wa dhana ya usemezano inayohusishwa na mwanaisimu, mwanafasihi na mwanafalsafa wa Kirusi, Mikhail Mikhailovich&nbsp; Bakhtin. Makala hii imebainisha sifa na viwango mbalimbali vya udhihirikaji huo wa mwingiliano na kuzungumzia athari zake katika&nbsp; uendelezaji wa maana ya kifasihi na fasiri za kifasihi zinazofuatia.&nbsp;</p> 2025-03-11T00:00:00+00:00 Copyright (c) 2025 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/290877 Mabadiliko ya Utambulisho wa Mwanamke na Uimarishaji wa Ujinsuke: Mifano kutoka Riwaya ya Nyuso za Mwanamke (Mohamed, 2010) 2025-03-11T11:12:21+00:00 Ernesta S. Mosha emosha904@gmail.com <p>Tafiti mbalimbali kuhusu riwaya ya Kiswahili zinaonesha kuwa mwanamke amesawiriwa kwa mitazamo mbalimbali, ukiwamo mtazamo&nbsp; hasi. Usawiri wa mtazamo huo unamtambulisha mwanamke kama kiumbe dhaifu na duni. Kwa kuongozwa na Nadharia ya Udenguzi,&nbsp; makala imeonesha namna mhusika mwanamke anavyoweza kubadilisha utambulisho hasi na kujenga utambulisho chanya. Makala imetumia data kutoka katika riwaya ya Nyuso za Mwanamke (Mohamed, 2010) zilizopatikana kwa usomaji makini. Makala imeweka&nbsp; bayana nafasi ya riwaya ya Kiswahili katika kujenga utambulisho wa mwanamke unaoimarisha ujinsuke2 . Matokeo haya yanatokana na&nbsp; uumbaji wa wahusika wanawake wanaodengua kaida za jamii zinazomkandamiza mwanamke na kufichua mbinu zinazotumiwa na&nbsp; baadhi ya wanajamii kuendeleza ukandamizaji huo. Pia, umuhimu wa wanawake kujitambua na kujisimamia umewekwa bayana.&nbsp;&nbsp;</p> 2025-03-11T00:00:00+00:00 Copyright (c) 2025 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/290879 Tofauti za Kifonolojia na Kimsamiati baina ya Kiswahili cha Kigoma, Ujiji na Kiswahili Sanifu 2025-03-11T11:32:36+00:00 Ahmad Y. Sovu sovu82@gmail.com <p>Watanzania wengi, hususani waishio vijijini, wana lugha zao za asili ambapo hujifunza Kiswahili na kukitumia kama lugha ya pili. Watanzania hao, wanapotumia Kiswahili huonekana wakibadili baadhi ya sauti na maneno. Makala hii inalenga kuchunguza tofauti za kifonolojia na kimsamiati baina ya Kiswahili cha Kigoma Ujiji na Kiswahili sanifu ili kubaini tofauti za matumizi ya sauti na maneno kati ya&nbsp; lugha hizo. Data zimekusanywa kwa kutumia ushuhudiaji na majadiliano ya vikundi. Uchambuzi na uwasilishaji wa data umeongozwa na&nbsp; Mkabala wa Mbinu Linganishi (Anttila, 1972). Matokeo ya uchunguzi yanaonesha kuwa kuna tofauti ya kifonolojia baina Kiswahili cha&nbsp; Kigoma, Ujiji na Kiswahili sanifu katika sauti zenye maneno yenye asili ya kigeni kama vile sauti [h], [bu], [mu]. Pia, kuna tofauti ya&nbsp; mabadiliko ya sauti [a] badala ya sauti [ha], [s] kuwa [sh], [r] badala ya [l], [bh] badala ya [b] na [bu] au [tu] kuwa [wa]. Aidha, kuna tofauti&nbsp; za matumizi ya sauti [-ga], lafudhi na mabadiliko ya kialami [ngo] badala ya sauti [eti] na tofauti za urefushaji irabu. Katika&nbsp; muktadha huo, Kiswahili cha Kigoma, Ujiji kinafanana na kutofautiana na Kiswahili sanifu kifonolojia na kimsamiati. Hata hivyo, tofauti&nbsp; zilizobainika ni zile za ubadilishaji wa sauti na msamiati usio wa msingi katika lugha hizo ambazo kwa kiasi kikubwa zinatokana na athari&nbsp; za lugha mama.&nbsp;&nbsp;</p> 2025-03-11T00:00:00+00:00 Copyright (c) 2025 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/290880 Uchanganyaji Msimbo katika Jamiilugha za Mitandaopepe:Mtagusano wa Kiswahili na Kiingereza 2025-03-11T11:43:29+00:00 Rhoda P. Kidami rhodapeterson@udsm.ac.tz <p>Mitandaopepe2 imetoa fursa kwa watu kutagusana katika masuala anuwai ya kijamii. Kiswahili ni miongoni mwa lugha zinazotumiwa katika mitandaopepe, ndani na nje ya Tanzania. Kutokana na kukua na kusambaa kwa lugha hiyo ulimwenguni kote, kuna haja ya&nbsp; kuchunguza mwonekano wake katika muktadha huo wa kimawasilianopepe. Lengo la makala hii ni kuchunguza jinsi Kiswahili&nbsp; kinavyotagusana na lugha ya Kiingereza katika mawasiliano hayo, hususani kwenye kipengele cha uchanganyaji msimbo. Data za utafiti&nbsp; huu ni maoni yaliyotolewa kwenye mtandao wa YouTube baada ya watu kusikiliza hotuba za Kiswahili za Mwalimu Nyerere. Jumla ya&nbsp; maoni elfu mbili na sitini yalikusanywa kutoka katika hotuba tatu. Uchanganuzi wa data hizo uliongozwa na Kiolezo cha Myers-Scotton&nbsp; (2001) kinachohusu lugha msingi na lugha changiaji katika kipengele cha uchanganyaji msimbo. Matokeo ya utafiti yamedhihirisha&nbsp; kwamba lugha za Kiswahili na Kiingereza zinakamilishana katika muktadha wa kimawasilianopepe. Katika miktadha tofautitofauti, lugha&nbsp; mojawapo imetumiwa kuwa msingi wa mawasiliano huku nyingine ikijaliza sarufi ya lugha msingi. Wakati mwingine, lugha zote mbili&nbsp; zimetumiwa kwa pamoja huku kila moja ikijikamilisha kisarufi.&nbsp;</p> 2025-03-11T00:00:00+00:00 Copyright (c) 2025 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/290881 Mwelekeo wa Usarufishaji wa Nomino za Kiswahili zenye Asili ya Kiingereza na Kiarabu 2025-03-11T11:47:42+00:00 Johari Hakimu jhakimu@mzumbe.ac.tz <p>Makala hii inaonesha mwelekeo wa usarufishaji wa nomino za Kiswahili zenye asili ya Kiingereza na Kiarabu. Mwelekeo wa nomimo hizo&nbsp; umeoneshwa kwa kutumia data iliyokusanywa kwa njia ya upitiaji wa nyaraka. Nyaraka zilizopitiwa ni Kamusi Kuu ya Kiswahili (2022) na&nbsp; Kamusi ya Karne ya 21 (2021). Data iliyopatikana ilichanganuliwa kwa kutumia Nadharia ya Mofolojia ya Ongezeko la Maneno na kufafanuliwa kwa kutumia Nadharia ya Usarufishaji. Uchanganuzi na ufafanuzi wa data hizo umeonesha kuwa kuna mielekeo chanya na&nbsp; hasi ya usarufishaji wa nomino za Kiswahili kwa kuzingatia ngeli za majina. Mwelekeo chanya wa usarufishaji wa nomino za Kiswahili zenye asili ya Kiingereza na Kiarabu umeonesha mchakato wa usarufishaji uliokamilika katika Kiswahili. Mwelekeo hasi umedhihirisha&nbsp; usarufishaji usiokamilika katika baadhi ya nomino za Kiswahili zenye asili ya Kiingereza na Kiarabu. Kwa ujumla, ufafanuzi wa nomino za&nbsp; Kiswahili unapaswa kuzingatia mazingira ya namna zinavyojitokeza na kusarufishwa katika lugha hii.&nbsp;&nbsp;</p> 2025-03-11T00:00:00+00:00 Copyright (c) 2025 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/290882 Phonological Nativisation of Swahili Loanwords in the Nyakyusa Language 2025-03-11T11:55:54+00:00 Andwele M. Mwakasege andwelemwakasege2@gmail.com <p>This paper examines the phonological nativisation processes of Swahili loanwords in the Nyakyusa language. The study was conducted in Rungwe district, in Mbeya region. The data were collected through the Nyakyusa written texts, elicitation guides, and observation of&nbsp; native speakers‟ conversations. The study adopted the theory of Assimilation propagated by Clements (1985). The theory advocates that&nbsp; when two speech communities are in contact for a considerable amount of time, they end up inter-influencing each other where the&nbsp; borrowed lexicons from the recipient language are adopted or undergo some modifications. It was evident that Nyakyusa, the&nbsp; beneficiary language, uses epenthesis and substitution as fixed procedures for lexicons not well shaped to influence them to fit in with&nbsp; the acquiring rules. More importantly, the findings revealed that with regard to borrowing, the Nyakyusa language has changed its&nbsp; phonological structure by introducing new consonants and allowing consonant clusters. The study recommends further studies on&nbsp; phonological nativisation processes in other districts where Nyakyusa is spoken as a native language, such as Kyela district and in other&nbsp; Bantu languages.&nbsp;</p> 2025-03-11T00:00:00+00:00 Copyright (c) 2025 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/290883 Ujitokezaji na Dhima za Yambwa katika Muundo wa Utendea wa Kimatengo na Kiswahili 2025-03-11T12:03:03+00:00 Fokas Nchimbi fokanchimbi@gmail.com <p>Miundo mbalimbali ya vitenzi vya lugha za Kibantu huweza kuamua ruwaza za utokeaji na dhima za kisemantiki za nomino za yambwa. Makala hii inachunguza mazingira ya utokeaji wa nomino za yambwa na dhima zake za kisemantiki katika lugha za Kimatengo na&nbsp; Kiswahili katika muundo wa kati wa utendea. Kufikia malengo hayo, makala hii inaongozwa na Nadharia ya Sarufi ya Uamilifu wa&nbsp; Kileksika inayomakinikia miundo miwili ya kisintaksia, yaani muundo wa kisintaksia unaowasilisha mfuatano wa maneno na makundi ya&nbsp; virai. Pili, muundo wa kisintaksia unaowasilisha uamilifu wa kisintaksia, kama vile kiima na yambwa. Data za utafiti huu zilikusanywa kwa&nbsp; njia kuu mbili. Data zinazohusu lugha ya Kimatengo zilipatikana uwandani kwa kuwatumia wazungumzaji asilia wa lugha hiyo. Data za&nbsp; Kiswahili zilikusanywa kutoka katika matini mbalimbali. Matokeo ya utafiti huu yanaonesha kuwapo kwa aina mbili za yambwa katika&nbsp; muundo wa utendea katika Kimatengo na Kiswahili, yaani yambwa tendewa na yambwa tendwa. Yambwa hizo zinazojitokeza baada ya&nbsp; kitenzi tendea zina dhima mbalimbali za kisemantiki ambazo ni unufaika, uathirika, uelekeo, kifaa na sababu.&nbsp;</p> 2025-03-11T00:00:00+00:00 Copyright (c) 2025 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/290886 Michakato ya Kisintaksia ya Uundaji wa Sentensi Changamani za Kiswahili 2025-03-11T12:53:12+00:00 Sephania M. Kyungu kombeluinasia@gmail.com Luinasia E. Kombe kombeluinasia@gmail.com <p>Makala hii inalenga kuchambua michakato ya kisintaksia ya uundaji wa sentensi changamani za Kiswahili kwa kubainisha namna kishazi kikuu na kishazi bebwa vinavyowekwa pamoja kuunda sentensi hizo. Ili kufanikisha lengo hilo, makala imeongozwa na Nadharia Rasmi ya Chomsky (1965). Data za makala hii ni sentensi changamani za Kiswahili ambazo zilikusanywa kwa njia ya usomaji wa matini kutoka katika riwaya na magazeti. Matini hizi ziliteuliwa kwa kutumia mbinu ya usampulishaji nasibu sahili. Uchambuzi wa data ulifanyika kwa mkabala wa kitaamuli kwa kutumia mbinu ya uchambuzi wa kimaudhui. Makala hii imebaini kwamba kuna michakato mitatu inayotumika&nbsp; kuunda sentensi changamani ambayo ni uchopekaji, udondoshaji-chopezi na udondoshaji-chopezi hamishi. Kwa kutumia Nadharia Rasmi, imebainika kwamba kila mchakato una hatua zake katika kuunda sentensi changamani.</p> 2025-03-11T00:00:00+00:00 Copyright (c) 2025 https://www.ajol.info/index.php/kcl/article/view/290888 Segmental Assimilation and Advanced Tongue Root Harmony in igiHa: An Autosegmental Phonological Analysis 2025-03-11T12:59:28+00:00 Saul S. Bichwa saul.bichwa@udsm.ac.tz <p>This study investigates phonological processes of segmental assimilation in igiHa, focusing on processes like nasalization, vowel harmony&nbsp; and homorganic nasal assimilation. The rationale stems from the need to document and analyse igiHa‘s phonological&nbsp; structures, especially Advanced Tongue Root (ATR) harmony, which has been underexplored in lesser-known Bantu languages.&nbsp; Autosegmental Phonology, a framework that separates phonological features across different tiers, serves as the theoretical foundation&nbsp; for analysing how segmental features spread between adjacent phonemes. Methodologically, the study employs introspective data&nbsp; collection supplemented by consultations with native speakers, following an elicitation approach to gather robust data on phonological acceptability. Findings reveal that igiHa uses feature spreading as a phonological mechanism, where assimilation occurs through ATR harmony, dividing vowels into [+ATR] and [-ATR] classes. Additionally, nasalization and homorganic nasal assimilation are significant in&nbsp; igiHa, with nasal consonants influencing adjacent vowels and consonants adapting to match the place of articulation of subsequent&nbsp; sounds. This study contributes to the field by elucidating the nuanced interplay of segmental features in igiHa, enhancing understanding&nbsp; of ATR harmony and feature assimilation in Bantu phonology.&nbsp;</p> 2025-03-11T00:00:00+00:00 Copyright (c) 2025