Main Article Content
KISWAHILI KWA KUFUNDISHIA: SERA NA MIKAKATI
Abstract
Pia, makala yanaeleza mambo muhimu katika utekelezaji wa sera mpya ya elimu. Baadhi ya mambo hayo ni: tamko rasmi la kutumia Kiswahili kama lugha ya kufundishia sekondari na vyuo, uimarishaji wa ufundishaji wa lugha ya Kiingereza, uandaaji wa mitaala na uandaaji wa semina mbalimbali zitakazotoa msingi kwa walimu wa lugha ya Kiswahili.
Makala yanahitimisha kwa kueleza kuwa, utekelezaji wa sera mpya una mambo yafuatayo ambayo ni muhimu; tamko la sera, ushiriki wa wanajamii katika kutumia lugha, vyombo vya ukuzaji lugha pamoja na wataalam wa lugha.