Main Article Content

Epistemolojia ya Waafrika katika Semi Zilizoandikwa kwenye Vazi la Kanga za Waswahili


Martina Duwe

Abstract

Epistemolojia ya Waafrika, wakiwamo Waswahili hubainika kupitia sanaa inayobeba mitazamo inayozingatiwa katika jamii yao. Moja kati  ya mambo yanayobainisha sanaa ya Waswahili ni vazi la kanga. Kwa jumla, usanaa katika vazi hilo hudhihirika kupitia maumbo au  michoro na lugha ya kiufundi ambayo hubeba semi kama vile, mafumbo, methali na misemo. Vazi la kanga huthaminiwa na hutumiwa  kwa namna mbalimbali katika maisha ya Waswahili, mathalani, kufunga kiunoni, kichwani, kujifunika na kama pambo (Hanby na Bygott,  1984). Kwa jumla, semi zilizoandikwa kwenye vazi la kanga zimefafanuliwa zaidi katika muktadha wa dhamira na dhima pasipo  kumakinikiwa kwa kina katika muktadha wa kiepistemolojia kulingana na kaida za Waswahili wenyewe. Makala haya yanafafanua namna  semi hizo zinavyobeba na kuhifadhi maarifa ya kiepistemolojia yanayosawiri maisha halisi ya Waswahili. Vilevile, misingi ya Nadharia ya  Sosholojia ya Kifasihi imetumika kama mwegamo mkuu katika kuchunguza, kuchanganua na kuwasilisha data husika. Matokeo  yanaonesha kuwa maandishi yaliyopo katika vazi la kanga yanahifadhi fasihi ya Waswahili, hususani semi ambazo hubainisha maarifa  mbalimbali, yakiwemo ya kiepistemolojia. Hivyo, makala haya yanajadili baadhi ya vipengele hivyo ambavyo ni: maarifa kuhusu kuwapo  kwa kani kuu, thamani ya kazi, heshima na utiifu na uvumilivu. 


Journal Identifiers


eISSN: 2958-4914