Main Article Content

Mtazamo wa Ki-Afrika katika Nadharia za Tafsiri


Hadija Jilala

Abstract

Makala haya yanahusu Mtazamo wa Ki-Afrika katika Nadharia za Tafsiri. Inafahamika kuwa chimbuko la nadharia za tafsiri zilizopo ni nchi  za Kimagharibi. Hata hivyo, katika nchi za Afrika taaluma ya tafsiri imepiga hatua kubwa ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kuwa na  wataalamu na wanataaluma wengi wa tafsiri, kufundishwa katika shule za sekondari, vyuo vya kati na vyuo vikuu. Pamoja na maendeleo  hayo, mpaka sasa hakuna nadharia ya tafsiri iliyobuliwa kupitia mazingira, muktadha na utamaduni wa lugha ya Kiswahili kama lugha ya Ki-Afrika. Hivyo, makala haya yanalenga kujadili umuhimu wa kuunda nadharia za tafsiri kwa kutumia muktadha wa lugha za Ki-Afrika na  kupendekeza hatua zitakazochukuliwa katika mchakato wa kuunda nadharia za tafsiri za Kiswahili. Makala yanajadili kwamba, pamoja na  kuwapo kwa nadharia zilizoibuliwa na wanazuoni wa Kimagharibi, kuna umuhimu wa kuunda nadharia za tafsiri ambazo zimefungamana  na muktadha, mazingira, mila, desturi, historia, lugha na utamaduni wa Ki-Afrika. Hii ni kwa sababu tafsiri hushughulika  na lugha ambayo ni mali ya jamii yenye utamaduni mahususi. Hivyo, nadharia za tafsiri zilizofumbata mtazamo wa Ki-Afrika zitakuwa  msingi, dira na mwongozo wa kinadharia na kivitendo katika kushughulikia tafsiri za matini mbalimbali za lugha za Ki-Afrika, hasa  zinazohusu dhana za kiutamaduni na fasihi. Vilevile nadharia hizo zitakuwa ni suluhisho la matatizo na changamoto za tafsiri kiisimu, kisemantiki, kiutamaduni na kifasihi. Makala haya yanapendekeza kuwa nadharia za tafsiri zinaweza kuundwa kwa kutumia mbinu  mbalimbali kama vile kuunda nadharia mpya, kuasili nadharia zilizopo na kuziboresha nadharia hizo. 


Journal Identifiers


eISSN: 2958-4914